Ayubu 29:7-17
7
“Wakati nilipokwenda kwenye lango la mji na kuketi katika kiwanja,
8
vijana waliniona wakakaa kando, nao wazee walioketi wakasimama;
9
wakuu wakaacha kuzungumza na kuziba vinywa vyao kwa mikono yao;
10
wenye vyeo wakanyamazishwa, nazo ndimi zao zikagandamana na makaakaa ya vinywa vyao.
11
Yeyote aliyenisikia alinena mema juu yangu, nao walioniona walinisifu,
12
kwa sababu nilimwokoa maskini aliyeomba msaada, naye yatima aliyekuwa hana wa kumsaidia.
13
Mtu aliyekuwa karibu kufa alinibariki, nami niliufanya moyo wa mjane kuimba.
14
Niliivaa haki kama vazi langu; uadilifu ulikuwa joho langu na kilemba changu.
15
Nilikuwa macho ya kipofu na miguu kwa kiwete.
16
Nilikuwa baba kwa mhitaji; nilimtetea mgeni.
17
Niliyavunja meno makali ya waovu, na kuwapokonya wahanga kwenye meno yao.
Settings