Ayubu 18:5
Inaonyesha mstari 5 pamoja na muktadha unaouzunguka.
2
“Je, ni lini utafika mwisho wa maneno haya? Uwe mwenye busara, nasi ndipo tutakapoweza kuongea.
3
Kwa nini sisi tunafikiriwa kama wanyama, na kuonekana wajinga machoni pako?
4
Wewe unayejirarua mwenyewe vipande vipande katika hasira yako, je, dunia iachwe kwa ajili yako wewe? Au ni lazima miamba iondolewe mahali pake?
5
“Taa ya mwovu imezimwa, nao mwali wa moto wake umezimika.
6
Mwanga hemani mwake umekuwa giza; taa iliyo karibu naye imezimika.
7
Nguvu za hatua zake zimedhoofishwa; shauri lake baya litamwangusha.
8
Miguu yake imemsukumia kwenye wavu, naye anatangatanga kwenye matundu ya wavu.
Settings