Ayubu 18:1-4
1
Bildadi Mshuhi akajibu:
2
“Je, ni lini utafika mwisho wa maneno haya? Uwe mwenye busara, nasi ndipo tutakapoweza kuongea.
3
Kwa nini sisi tunafikiriwa kama wanyama, na kuonekana wajinga machoni pako?
4
Wewe unayejirarua mwenyewe vipande vipande katika hasira yako, je, dunia iachwe kwa ajili yako wewe? Au ni lazima miamba iondolewe mahali pake?
Settings