Rukia maudhui
Mwanzo 24:62-67

Isaka na Rebeka wakutana

Mwanzo 24:62-67
62
Basi Isaki alikuwa ametoka Beer-Lahai-Roi, kwa kuwa alikuwa anaishi nchi ya Negebu.
63
Isaki akatoka kwenda shambani kutafakari wakati wa jioni, alipoinua macho yake, akaona ngamia wanakuja.
64
Rebeka pia akainua macho akamwona Isaki. Akashuka kutoka kwenye ngamia wake
65
na akamuuliza yule mtumishi, “Ni nani mtu yule aliye kule shambani anayekuja kutulaki?” Yule mtumishi akajibu, “Huyu ndiye bwana wangu.” Hivyo Rebeka akachukua shela yake akajifunika.
66
Kisha yule mtumishi akamweleza Isaki mambo yote aliyoyatenda.
67
Ndipo Isaki akamwingiza Rebeka katika hema la Sara mama yake, Isaki akamchukua Rebeka, hivyo akawa mke wake. Isaki akampenda, akafarijika baada ya kifo cha mama yake.
Settings

Reading Style

Typeface

Font Size 19px

Reading Width 45 chars

Options