Rukia maudhui
Waefeso 6:1-9

Waefeso 6:1-9

1
Enyi watoto, watiini wazazi wenu katika Bwana, kwa kuwa hili ni jema.
2
“Waheshimu baba yako na mama yako,” hii ndio amri ya kwanza yenye ahadi,
3
“upate baraka na uishi siku nyingi duniani.”
4
Ninyi akina baba, msiwachokoze watoto wenu, bali waleeni kwa nidhamu na mafundisho ya Bwana.
5
Ninyi watumwa, watiini hao walio mabwana zenu hapa duniani kwa heshima na kwa kutetemeka na kwa moyo mmoja, kama vile mnavyomtii Kristo.
6
Watiini, si tu wakati wakiwaona ili mpate upendeleo wao, bali mtumike kama watumwa wa Kristo, mkifanya mapenzi ya Mungu kwa moyo.
7
Tumikeni kwa moyo wote, kama vile mnamtumikia Bwana na si wanadamu.
8
Mkijua kwamba Bwana atampa kila mtu thawabu kwa lolote jema alilotenda, kama yeye ni mtumwa au ni mtu huru.
9
Nanyi mabwana, watendeeni watumwa wenu kwa jinsi iyo hiyo. Msiwatishe, kwa kuwa mnajua ya kwamba yeye aliye Bwana wenu na Bwana wao yuko mbinguni, naye hana upendeleo.
Settings

Reading Style

Typeface

Font Size 19px

Reading Width 45 chars

Options