Skip to content
1 Nyakati 6:16-49

1 Nyakati 6:16-49

16
Wana wa Lawi walikuwa: Gershoni, Kohathi na Merari.
17
Haya ndiyo majina ya wana wa Gershoni: Libni na Shimei.
18
Wana wa Kohathi walikuwa: Amramu, Ishari, Hebroni na Uzieli.
19
Wana wa Merari walikuwa: Mahli na Mushi. Zifuatazo ni koo za Walawi zilizoorodheshwa kufuatana na baba zao:
20
Wazao wa Gershoni: Gershoni akamzaa Libni, Libni akamzaa Yahathi, Yahathi akamzaa Zima,
21
Zima akamzaa Yoa, Yoa akamzaa Ido, Ido akamzaa Zera, Zera akamzaa Yeatherai.
22
Wazao wa Kohathi: Kohathi akamzaa Aminadabu, Aminadabu akamzaa Kora, Kora akamzaa Asiri,
23
Asiri akamzaa Elikana, Elikana akamzaa Ebiasafu, Ebiasafu akamzaa Asiri,
24
Asiri akamzaa Tahathi, Tahathi akamzaa Urieli, Urieli akamzaa Uzia, Uzia akamzaa Shauli.
25
Wazao wa Elikana walikuwa: Amasai na Ahimothi,
26
Ahimothi akamzaa Elikana, Elikana akamzaa Sofai, Sofai akamzaa Nahathi,
27
Nahathi akamzaa Eliabu, Eliabu akamzaa Yerohamu, Yerohamu akamzaa Elikana, Elikana akamzaa Samweli.
28
Wana wa Samweli walikuwa: Yoeli mzaliwa wake wa kwanza, na Abiya mwanawe wa pili.
29
Wafuatao ndio wazao wa Merari: Merari akamzaa Mahli, Mahli akamzaa Libni, Libni akamzaa Shimei, Shimei akamzaa Uza,
30
Uza akamzaa Shimea, Shimea akamzaa Hagia, Hagia akamzaa Asaya.
31
Hawa ndio watu ambao Daudi aliwaweka kuwa viongozi wa uimbaji katika nyumba ya Bwana, baada ya Sanduku la Agano kuletwa ili kukaa huko.
32
Walihudumu kwa kuimba mbele ya Maskani, Hema la Kukutania, mpaka hapo Mfalme Solomoni alipojenga Hekalu la Bwana huko Yerusalemu. Walitimiza wajibu wao kulingana na taratibu walizokuwa wamewekewa.
33
Wafuatao ni watu waliohudumu pamoja na wana wao: Kutoka ukoo wa Kohathi walikuwa: Hemani, mpiga kinanda, alikuwa mwana wa Yoeli, mwana wa Samweli,
34
mwana wa Elikana, mwana wa Yerohamu, mwana wa Elieli, mwana wa Toa,
35
mwana wa Sufu, mwana wa Elikana, mwana wa Mahathi, mwana wa Amasai,
36
mwana wa Elikana, mwana wa Yoeli, mwana wa Azaria, mwana wa Sefania,
37
mwana wa Tahathi, mwana wa Asiri, mwana wa Ebiasafu, mwana wa Kora,
38
mwana wa Ishari, mwana wa Kohathi, mwana wa Lawi, mwana wa Israeli;
39
na msaidizi wa Hemani alikuwa Asafu, aliyesimama mkono wa kuume: Asafu mwana wa Berekia, mwana wa Shimea,
40
mwana wa Mikaeli, mwana wa Baaseya, mwana wa Malkiya,
41
mwana wa Ethni, mwana wa Zera, mwana wa Adaya,
42
mwana wa Ethani, mwana wa Zima, mwana wa Shimei,
43
mwana wa Yahathi, mwana wa Gershoni, mwana wa Lawi.
44
Na kutoka kwa walioshirikiana nao, Wamerari, mkono wake wa kushoto: Ethani mwana wa Kishi, mwana wa Abdi, mwana wa Maluki,
45
mwana wa Hashabia, mwana wa Amazia, mwana wa Hilkia,
46
mwana wa Amsi, mwana wa Bani, mwana wa Shemeri,
47
mwana wa Mahli, mwana wa Mushi, mwana wa Merari, mwana wa Lawi.
48
Ndugu zao wengine Walawi walipewa huduma nyingine za kuhudumia hema takatifu, nyumba ya Mungu.
49
Lakini Aroni na uzao wake ndio waliokuwa na wajibu wa kutoa sadaka katika madhabahu ya sadaka ya kuteketezwa na kwenye madhabahu ya kufukizia uvumba pamoja na yote yaliyofanyika pa Patakatifu, wakifanya upatanisho kwa ajili ya Israeli, sawasawa na yale yote aliyoagiza Mose mtumishi wa Mungu.
Settings

Reading Style

Typeface

Font Size 19px

Options