1 Nyakati 6:1-15
1
Wana wa Lawi walikuwa: Gershoni, Kohathi na Merari.
2
Wana wa Kohathi walikuwa: Amramu, Ishari, Hebroni na Uzieli.
3
Amramu alikuwa na wana: Aroni, Mose, na Miriamu. Aroni alikuwa na wana: Nadabu, Abihu, Eleazari na Ithamari.
4
Eleazari akamzaa Finehasi, Finehasi akamzaa Abishua,
5
Abishua akamzaa Buki, Buki akamzaa Uzi,
6
Uzi akamzaa Zerahia, Zerahia akamzaa Merayothi,
7
Merayothi akamzaa Amaria, Amaria akamzaa Ahitubu,
8
Ahitubu akamzaa Sadoki, Sadoki akamzaa Ahimaasi,
9
Ahimaasi akamzaa Azaria, Azaria akamzaa Yohanani,
10
Yohanani akamzaa Azaria (ndiye alifanya kazi ya ukuhani katika Hekalu alilojenga Mfalme Solomoni huko Yerusalemu),
11
Azaria akamzaa Amaria, Amaria akamzaa Ahitubu,
12
Ahitubu akamzaa Sadoki, Sadoki akamzaa Shalumu,
13
Shalumu akamzaa Hilkia, Hilkia akamzaa Azaria,
14
Azaria akamzaa Seraya, Seraya akamzaa Yehosadaki.
15
Yehosadaki alihamishwa wakati Bwana aliwapeleka uhamishoni watu wa Yuda na Yerusalemu kwa mkono wa Mfalme Nebukadneza.
Settings