- English
- King James KJV
- Complete Jewish CJB
- World English WEBM
- Berean Standard BSB
- American Standard ASV
- Geneva GNV
- Young's Literal YLT
- Douay-Rheims DRC
- International
- Shqip ALB
- العربية SVD
- বাংলা BN-IRV
- မြန်မာ Judson
- 简体文 CUV-S
- 繁體中文 CUV-T
- Čeština BKR
- Nederlands STVE
- Français LSG
- Deutsch SCH
- Ελληνικά Vamvas
- ગુજરાતી GU-IRV
- Hausa HCB
- עברית Hebrew
- हिन्दी HCV
- Magyar KAROLI
- Bahasa Indonesia INDO-TB
- Italiano Diodati
- 日本語 Kougo
- 한국어 Korean
- മലയാളം MAL
- मराठी MRCV
- Norsk DNB
- فارسی OPV
- Polski BG
- Português Almeida
- Română Cornilescu
- Русский Synodal
- Español RVG
- Kiswahili Neno
- Svenska SV1917
- Tagalog TAG-ADB
- தமிழ் TCV
- తెలుగు TSA
- ภาษาไทย THAI-KJV
- Українська Ohienko
- Tiếng Việt CADMAN
- Yorùbá YCB
Zaburi116
Listen to this chapter
0:00
0:00
Tamko la Kumpenda BWANA
1
Ninampenda Bwana kwa maana amesikia sauti yangu; amesikia kilio changu ili anihurumie.
2
Kwa sababu amenitegea sikio lake, nitamwita siku zote za maisha yangu.
Kukumbuka Taabu na Maombi ya Kukata Tamaa
3
Kamba za mauti zilinizunguka, maumivu makuu ya kuzimu yalinipata, nikalemewa na taabu na huzuni.
4
Ndipo nikaliitia jina la Bwana: “Ee Bwana, niokoe!”
Kutangaza Rehema na Haki ya Mungu
5
Bwana ni mwenye neema na haki, Mungu wetu ni mwingi wa huruma.
6
Bwana huwalinda wanyenyekevu, nilipokuwa katika shida kubwa, aliniokoa.
7
Ee nafsi yangu, tulia tena, kwa kuwa Bwana amekuwa mwema kwako.
8
Kwa kuwa wewe, Ee Bwana, umeniokoa nafsi yangu na mauti, macho yangu kutokana na machozi, miguu yangu kutokana na kujikwaa,
9
ili niweze kutembea mbele za Bwana, katika nchi ya walio hai.
Imani Iliyopimwa Katika Taabu
10
Niliamini, kwa hiyo nilisema, “Mimi nimeteseka sana.”
11
Katika taabu yangu nilisema, “Wanadamu wote ni waongo.”
Kushika Nadhiri na Ibada ya Hadhara
12
Nimrudishie Bwana nini kwa wema wake wote alionitendea?
13
Nitakiinua kikombe cha wokovu na kulitangaza jina la Bwana.
14
Nitazitimiza nadhiri zangu kwa Bwana mbele za watu wake wote.
15
Kifo cha watakatifu kina thamani machoni pa Bwana.
16
Ee Bwana, hakika mimi ni mtumishi wako, mimi ni mtumishi wako, mwana wa mjakazi wako; umeniweka huru toka katika minyororo yangu.
17
Nitakutolea dhabihu ya kukushukuru na kuliita jina la Bwana.
18
Nitazitimiza nadhiri zangu kwa Bwana mbele za watu wake wote,
19
katika nyua za nyumba ya Bwana, katikati yako, ee Yerusalemu. Msifuni Bwana.
Use ← → arrow keys to navigate
Settings
Reading Style
Typeface
Font Size px
Reading Width chars
Options
Study Note