Rukia maudhui

Ayubu25

Hotuba ya mwisho fupi ya Bildadi

1
Ndipo Bildadi Mshuhi akajibu:

Utawala kamili wa Mungu

2
“Mamlaka na kuheshimiwa ni vyake Mungu; yeye huthibitisha amani katika mbingu juu.
3
Je, majeshi yake yaweza kuhesabika? Ni nani asiyeangaziwa na nuru yake?

Uchafu wa wanadamu

4
Mtu awezaje kuwa mwadilifu mbele za Mungu? Awezaje mtu aliyezaliwa na mwanamke kuwa safi?
5
Ikiwa hata mwezi sio mwangavu nazo nyota si safi machoni pake,
6
sembuse mtu ambaye ni funza: mwanadamu ambaye ni buu tu!”
Use arrow keys to navigate
Settings

Reading Style

Typeface

Font Size 19px

Reading Width 45 chars

Options