Mistari ya Biblia kuhusu The Tribes of Israel: Under a president or chief
Mistari kuhusu Under a president or chief
Mwanaume mmoja kutoka kila kabila, kila aliye kiongozi wa jamaa yake, atawasaidia.
Haya ndiyo majina ya wanaume watakaowasaidia: “kutoka Reubeni, ni Elisuri mwana wa Shedeuri;
kutoka Simeoni, ni Shelumieli mwana wa Surishadai;
kutoka Yuda, ni Nashoni mwana wa Aminadabu;
kutoka Isakari, ni Nethaneli mwana wa Suari;
kutoka Zabuloni, ni Eliabu mwana wa Heloni;
kutoka wana wa Yosefu: kutoka Efraimu, ni Elishama mwana wa Amihudi; kutoka Manase, ni Gamalieli mwana wa Pedasuri;
kutoka Benyamini, ni Abidani mwana wa Gideoni;
kutoka Dani, ni Ahiezeri mwana wa Amishadai;
kutoka Asheri, ni Pagieli mwana wa Okrani;
kutoka Gadi, ni Eliasafu mwana wa Deueli;
kutoka Naftali, ni Ahira mwana wa Enani.”
Hawa walikuwa wanaume walioteuliwa kutoka jumuiya, viongozi wa makabila ya baba zao. Walikuwa wakuu wa koo za Israeli.