Mistari ya Biblia kuhusu Seeking God: His being found
Mistari kuhusu His being found
Lakini kama mtamtafuta Bwana Mungu wenu, mtampata; kama mtamtafuta kwa moyo wenu wote na kwa roho yote.
“Nawe Solomoni mwanangu, mjue Mungu wa baba yako, ukamtumikie kwa kujitoa kwa moyo wote na kwa nia ya kumkubali, kwa maana Bwana huuchunguza kila moyo na kujua kila kusudi la kila fikira. Ukimtafuta, ataonekana kwako; bali kama ukimwacha, yeye atakukataa milele.
Nawapenda wale wanipendao, na wale wanitafutao kwa bidii wataniona.
Mtanitafuta na kuniona, mtakaponitafuta kwa moyo wenu wote.