Skip to content

Mistari ya Biblia kuhusu Obduracy: General references

20 mistari · 1 kipengele

Mistari kuhusu General references

  1. Bwana, Mungu wa baba zao, akawapelekea neno kupitia wajumbe wake tena na tena, kwa sababu alikuwa anawahurumia watu wake pamoja na mahali pa maskani yake.

  2. Lakini waliwadhihaki wajumbe wa Bwana wakayadharau maneno yake na kuwacheka manabii wake mpaka ghadhabu ya Bwana ikawa kubwa dhidi ya watu wake na hakukuwa na namna ya kuituliza.

  3. msiifanye mioyo yenu migumu kama mlivyofanya kule Meriba, kama mlivyofanya siku ile kule Masa jangwani,

  4. ambapo baba zenu walinijaribu na kunipima, ingawa walikuwa wameyaona matendo yangu.

  5. Kwa miaka arobaini nilikasirikia kizazi kile, nikasema, “Hawa ni taifa ambalo mioyo yao imepotoka, nao hawajazijua njia zangu.”

  6. Hivyo nikatangaza kwa kiapo katika hasira yangu, “Kamwe hawataingia rahani mwangu.”

  7. Lakini kwa kuwa mlinikataa nilipowaita na hakuna yeyote aliyekubali niliponyoosha mkono wangu,

  8. kwa kuwa mliyapuuza mashauri yangu yote na hamkukubali karipio langu,

  9. mimi nami nitawacheka katika maafa yenu, nitawadhihaki wakati janga litawapata:

  10. wakati janga litawapata kama tufani, wakati maafa yatawazoa kama upepo wa kisulisuli, wakati dhiki na taabu zitawalemea.

  11. “Ndipo watakaponiita lakini sitawajibu; watanitafuta lakini hawatanipata.

  12. Kwa kuwa walichukia maarifa, wala hawakuchagua kumcha Bwana,

  13. kwa kuwa hawakukubali mashauri yangu, na kukataa maonyo yangu,

  14. watakula matunda ya njia zao, na watashibishwa matunda ya hila zao.

  15. Mtu anayeendelea kuwa na shingo ngumu baada ya maonyo mengi, ataangamia ghafula, wala hapati dawa.

  16. msiifanye mioyo yenu migumu, kama mlivyofanya katika uasi, wakati ule wa kujaribiwa jangwani,

  17. Kama ilivyonenwa: “Leo, kama mkiisikia sauti yake, msiifanye mioyo yenu migumu kama mlivyofanya wakati wa kuasi.”

  18. Kwa hiyo Mungu ameweka siku nyingine, akaiita Leo, akisema kwa kinywa cha Daudi baadaye sana, kwa maneno yaliyotangulia kunenwa: “Leo, kama mkiisikia sauti yake, msiifanye mioyo yenu migumu.”

  19. Wanadamu waliosalia, ambao hawakuuawa katika mapigo hayo, bado walikataa kutubia kazi za mikono yao na hawakuacha kuabudu mashetani na sanamu za dhahabu, za fedha, za shaba, za mawe na za miti, ambazo haziwezi kuona, kusikia wala kutembea.

  20. Wala hawakutubu na kuacha matendo yao ya uuaji, uchawi, uasherati wala wizi wao.