Skip to content

Mistari ya Biblia kuhusu Geology: General references

21 mistari · 1 kipengele

Mistari kuhusu General references

  1. Mungu akasema, “Maji yaliyopo chini ya anga na yakusanyike mahali pamoja, pawepo na nchi kavu.” Ikawa hivyo.

  2. Mungu akaiita nchi kavu “ardhi,” nalo lile kusanyiko la maji akaliita “bahari.” Mungu akaona kuwa ni vyema.

  3. au zungumzeni na dunia, nayo itawafundisha, au acheni samaki wa baharini wawape taarifa.

  4. Ni nani miongoni mwa hawa wote asiyejua kwamba mkono wa Bwana ndio uliofanya hili?

  5. Mikono ya mwanadamu hushambulia miamba migumu sana, na kuiacha wazi mizizi ya milima.

  6. Hutoboa shimo refu la kupenya chini kwa chini kwenye miamba; macho yake huona hazina zake zote.

  7. Hutafuta vyanzo vya mito na kuvileta vitu vilivyofichika katika nuru.

  8. Zaburi ya Daudi. Dunia ni mali ya Bwana, na vyote vilivyomo ndani yake, ulimwengu, na wote waishio ndani yake,

  9. maana aliiwekea misingi yake baharini na kuifanya imara juu ya maji.

  10. Ameiweka dunia kwenye misingi yake, haiwezi kamwe kuondoshwa.

  11. Uliifunika kwa kilindi kama kwa vazi, maji yalisimama juu ya milima.

  12. Lakini kwa kukemea kwako maji yalikimbia, kwa sauti ya radi yako yakatoroka,

  13. yakapanda milima, yakateremka mabondeni, hadi mahali pale ulipoyakusudia.

  14. Uliyawekea mpaka ambao hayawezi kuuvuka, kamwe hayataifunika dunia tena.

  15. Huzifanya chemchemi zimwage maji mabondeni, hutiririka kati ya milima.

  16. Huwapa maji wanyama wote wa kondeni, punda-mwitu huzima kiu yao.

  17. Ndege wa angani hufanya viota kando ya maji, huimba katikati ya matawi.

  18. Huinyeshea milima kutoka orofa zake, dunia inatoshelezwa kwa matunda ya kazi yake.

  19. Lakini wao kwa makusudi hupuuza ukweli huu, ya kwamba kwa neno la Mungu mbingu zilikuwepo tangu zamani, nayo dunia ilifanyizwa kutoka ndani ya maji na kwa maji.

  20. Ulimwengu wa wakati ule uligharikishwa kwa hayo maji na kuangamizwa.

  21. Lakini kwa neno lilo hilo, mbingu za sasa na dunia zimewekwa akiba kwa ajili ya moto, zikihifadhiwa hadi siku ile ya hukumu na ya kuangamizwa kwa watu wasiomcha Mungu.