Rukia maudhui

Mistari ya Biblia kuhusu Baptism With the Holy Spirit

9 mistari · 9 vipengele

Mistari muhimu ya Biblia

  1. Siku ya Pentekoste ilipowadia, waamini wote walikuwa mahali pamoja.

  2. Ghafula sauti kama mvumo mkubwa wa upepo mkali uliotoka mbinguni ukaijaza nyumba yote walimokuwa wameketi.

  3. Zikatokea ndimi kama za moto zilizogawanyika na kukaa juu ya kila mmoja wao.

  4. Wote wakajazwa na Roho Mtakatifu, wakaanza kunena kwa lugha nyingine, kama Roho alivyowajalia.

  5. akawauliza, “Je, mlipokea Roho Mtakatifu mlipoamini?” Wakajibu, “Hapana, hata hatukusikia kuwa kuna Roho Mtakatifu.”

  6. Ndipo Paulo akawauliza, “Je, mlibatizwa kwa ubatizo gani?” Wakajibu, “Kwa ubatizo wa Yohana.”

  7. Paulo akasema, “Ubatizo wa Yohana ulikuwa wa toba, aliwaambia watu wamwamini yeye atakayekuja baada yake, yaani, Yesu.”

  8. Waliposikia haya, wakabatizwa katika jina la Bwana Yesu.

  9. Paulo alipoweka mikono yake juu yao, Roho Mtakatifu akawashukia, nao wakanena kwa lugha mpya na kutabiri.