- English
- King James KJV
- Complete Jewish CJB
- World English WEBM
- Berean Standard BSB
- American Standard ASV
- Geneva GNV
- Young's Literal YLT
- Douay-Rheims DRC
- International
- Shqip ALB
- العربية SVD
- বাংলা BN-IRV
- မြန်မာ Judson
- 简体文 CUV-S
- 繁體中文 CUV-T
- Čeština BKR
- Nederlands STVE
- Français LSG
- Deutsch SCH
- Ελληνικά Vamvas
- ગુજરાતી GU-IRV
- Hausa HCB
- עברית Hebrew
- हिन्दी HCV
- Magyar KAROLI
- Bahasa Indonesia INDO-TB
- Italiano Diodati
- 日本語 Kougo
- 한국어 Korean
- മലയാളം MAL
- मराठी MRCV
- Norsk DNB
- فارسی OPV
- Polski BG
- Português Almeida
- Română Cornilescu
- Русский Synodal
- Español RVG
- Kiswahili Neno
- Svenska SV1917
- Tagalog TAG-ADB
- தமிழ் TCV
- తెలుగు TSA
- ภาษาไทย THAI-KJV
- Українська Ohienko
- Tiếng Việt CADMAN
- Yorùbá YCB
Mistari ya Biblia kuhusu Atheism: Arguments against
Mistari kuhusu Arguments against
“Lakini ulizeni wanyama, nao watawafundisha, au ndege wa angani, nao watawaambia;
au zungumzeni na dunia, nayo itawafundisha, au acheni samaki wa baharini wawape taarifa.
Ni nani miongoni mwa hawa wote asiyejua kwamba mkono wa Bwana ndio uliofanya hili?
Mkononi mwake kuna uhai wa kila kiumbe, na pumzi ya wanadamu wote.
Je, sikio haliyajaribu maneno kama vile ulimi uonjavyo chakula?
Je, hekima haipatikani katikati ya wazee? Je, maisha marefu hayaleti ufahamu?
“Hekima na nguvu ni vya Mungu; shauri na ufahamu ni vyake yeye.
Kile anachokibomoa hakiwezi kujengeka tena; mtu aliyefungiwa naye hawezi kufunguliwa.
Akizuia maji, huwa pana ukame; akiyaachia maji, huharibu nchi.
Kwake kuna nguvu na ushindi; adanganywaye na adanganyaye, wote wawili ni wake.
Yeye huwaondoa washauri wakiwa wametekwa nyara, naye huwapumbaza wanaotoa maamuzi.
Huondoa pingu zilizofungwa na wafalme, na kuwafunga mishipi ya kiunoni.
Huwaondoa makuhani wakiwa wametekwa nyara, na kuwaangusha waliojiimarisha muda mrefu.
Hunyamazisha midomo ya washauri wanaoaminika, na kuondoa busara ya wazee.
Huwamwagia dharau wanaoheshimika, na kuwavua silaha wenye nguvu.
Hufunua mambo ya ndani ya gizani, na kuyaleta nuruni yale yaliyositirika sana.
Huyafanya mataifa yatukuke na kuyaangamiza; hufanya mataifa kuwa makubwa, naye huyatawanya.
Huwaondolea viongozi wa nchi akili zao; huwapeleka watangetange nyikani pasipo na njia.
Hupapasa gizani pasipokuwa na mwanga; huwafanya wapepesuke kama walevi.
kwa maana yote yanayoweza kujulikana kumhusu Mungu ni dhahiri kwao, kwa sababu Mungu mwenyewe ameyadhihirisha kwao.
Kwa maana tangu kuumbwa kwa ulimwengu, asili ya Mungu asiyeonekana kwa macho, yaani, uweza wake wa milele na asili yake ya Uungu, imeonekana waziwazi, ikitambuliwa kutokana na yale aliyoyafanya ili wanadamu wasiwe na udhuru.