Rukia maudhui

circa 1446–1406 BC

The Wilderness Years

Forty years of wandering in the desert test Israel's faith and prepare a new generation to enter the promised land.

2,247 mistari · 2 vitabu vimehusishwa

Mistari ya kipindi hiki

Chuja kwa kitabu
  1. Kumbukumbu 29:26takriban 1451 KK

    Walienda zao na kuabudu miungu mingine na kuisujudia, miungu wasioijua, miungu ambayo Mungu hakuwapa.

  2. Kumbukumbu 29:27takriban 1451 KK

    Kwa hiyo hasira ya Bwana ikawaka dhidi ya nchi hii, hivyo Mungu akaleta juu yake laana zote zilizoandikwa katika kitabu hiki.

  3. Kumbukumbu 29:28takriban 1451 KK

    Katika hasira kali na katika ghadhabu kuu Bwana aliwangʼoa kutoka nchi yao na kuwasukumia katika nchi nyingine, kama ilivyo sasa.”

  4. Kumbukumbu 29:29takriban 1451 KK

    Mambo ya siri ni ya Bwana Mungu wetu, bali yaliyofunuliwa ni yetu na watoto wetu milele, ili tuweze kuyafanya maneno yote ya sheria hii.

  5. Kumbukumbu 30:1takriban 1451 KK

    Wakati baraka hizi zote pamoja na laana nilizoziweka mbele yako zitakapokujia, nawe ukazitafakari moyoni popote Bwana Mungu wako atakapokutawanya miongoni mwa mataifa,

  6. Kumbukumbu 30:2takriban 1451 KK

    hapo wewe na watoto wako mtakapomrudia Bwana Mungu wako, na kumtii kwa moyo wako wote na kwa roho yako yote kulingana na kila kitu ninachokuamuru leo,

  7. Kumbukumbu 30:3takriban 1451 KK

    ndipo Bwana Mungu wako atakapokurudisha kutoka utumwani na kukuhurumia, naye atakukusanya tena kutoka mataifa yote kule alikutawanya.

  8. Kumbukumbu 30:4takriban 1451 KK

    Hata kama umefukuziwa katika nchi ya mbali kiasi gani chini ya mbingu, kutoka huko Bwana Mungu wako atakukusanya na kukurudisha.

  9. Kumbukumbu 30:5takriban 1451 KK

    Yeye Bwana atakurudisha katika nchi iliyokuwa mali ya baba zako, nawe utaimiliki. Naye atakufanya ufanikiwe sana na kukuzidisha kwa idadi kuliko baba zako.

  10. Kumbukumbu 30:6takriban 1451 KK

    Bwana Mungu wako ataitahiri mioyo yenu na mioyo ya wazao wenu ili mweze kumpenda kwa moyo wako wote na kwa roho yako yote ukaishi.

  11. Kumbukumbu 30:7takriban 1451 KK

    Bwana Mungu wako ataweka laana hizi zote juu ya adui zako ambao wanakuchukia na kukutesa.

  12. Kumbukumbu 30:8takriban 1451 KK

    Utamtii tena Bwana na kuzishika amri zake zote ninazokupa leo.

  13. Kumbukumbu 30:9takriban 1451 KK

    Ndipo Bwana Mungu wako atakapokufanikisha sana katika kazi zote za mikono yako na katika uzao wa tumbo lako, wadogo wa mifugo yako na mazao ya nchi yako. Bwana atakufurahia tena na kukufanikisha, kama alivyowafurahia baba zako,

  14. Kumbukumbu 30:10takriban 1451 KK

    kama ukimtii Bwana Mungu wako, na kuzishika amri zake na maagizo yake ambayo yameandikwa katika Kitabu hiki cha Sheria, na kumgeukia Bwana Mungu wako kwa moyo wako wote na kwa roho yako yote.

  15. Kumbukumbu 30:11takriban 1451 KK

    Ninachokuagiza leo sio kigumu sana kwako au usichokiweza.

  16. Kumbukumbu 30:12takriban 1451 KK

    Hakiko juu mbinguni, ili uulize, “Ni nani atakayepanda mbinguni kukileta na kututangazia ili tuweze kutii?”

  17. Kumbukumbu 30:13takriban 1451 KK

    Wala hakiko ngʼambo ya bahari, ili uulize, “Ni nani atakayevuka bahari kwenda kukichukua na kututangazia ili tupate kutii?”

  18. Kumbukumbu 30:14takriban 1451 KK

    La hasha! Lile neno liko karibu sana nawe; liko kinywani mwako na ndani ya moyo wako ili uweze kulitii.

  19. Kumbukumbu 30:15takriban 1451 KK

    Tazama, naweka mbele yako leo uzima na mafanikio, mauti na maangamizo.

  20. Kumbukumbu 30:16takriban 1451 KK

    Ninakuamuru leo kwamba umpende Bwana Mungu wako, utembee katika njia zake, na kutunza maagizo yake, amri na sheria zake; ndipo utakapoishi na kuongezeka, naye Bwana Mungu wako atakubariki katika nchi unayoingia kuimiliki.

  21. Kumbukumbu 30:17takriban 1451 KK

    Lakini kama moyo wako ukigeukia mbali ukawa huna utii, kama umevutwa kuisujudia miungu mingine na kuiabudu,

  22. Kumbukumbu 30:18takriban 1451 KK

    nakutangazia leo hii kwamba hakika utaangamizwa. Hutaishi maisha marefu katika nchi unayovuka Yordani kuiingia na kuimiliki.

  23. Kumbukumbu 30:19takriban 1451 KK

    Leo ninaziita mbingu na nchi kama mashahidi dhidi yako kwamba nimeweka mbele yako uzima na mauti, baraka na laana. Basi sasa chagueni uzima, ili wewe na watoto wako mpate kuishi,

  24. Kumbukumbu 30:20takriban 1451 KK

    na ili upate kumpenda Bwana Mungu wako, uisikilize sauti yake na kuambatana naye. Kwa kuwa Bwana ndiye uzima wako, na atakupa wingi wa siku ili upate kuishi katika nchi aliyoapa kuwapa baba zako Abrahamu, Isaki na Yakobo.

  25. Kumbukumbu 31:1takriban 1451 KK

    Kisha Mose akaenda akasema maneno haya kwa Waisraeli wote: