Rukia maudhui
Zaburi 69:7-12

Kuteswa kwa Ajili ya Mungu

Zaburi 69:7-12
7
Kwa maana nimestahimili dharau kwa ajili yako, aibu imefunika uso wangu.
8
Nimekuwa mgeni kwa ndugu zangu, mgeni kwa wana wa mama yangu mwenyewe.
9
Kwa kuwa wivu wa nyumba yako unanila, matukano ya wale wanaokutukana yameniangukia.
10
Ninapolia na kufunga, lazima nivumilie matusi.
11
Ninapovaa nguo ya gunia, watu hunidharau.
12
Wale wanaoketi mlangoni wananisimanga, nimekuwa wimbo wa walevi.
Settings

Reading Style

Typeface

Font Size 19px

Reading Width 45 chars

Options