Skip to content
Zaburi 44:9-16

Zaburi 44:9-16

9
Lakini sasa umetukataa na kutudhili, wala huendi tena na jeshi letu.
10
Umetufanya turudi nyuma mbele ya adui, nao watesi wetu wametuteka nyara.
11
Umetuacha tutafunwe kama kondoo na umetutawanya katika mataifa.
12
Umewauza watu wako kwa fedha kidogo, wala hukupata faida yoyote kwa mauzo yao.
13
Umetufanya lawama kwa jirani zetu, dharau na dhihaka kwa wale wanaotuzunguka.
14
Umetufanya kuwa mithali miongoni mwa mataifa, mataifa hutikisa vichwa vyao.
15
Fedheha yangu iko mbele yangu mchana kutwa, na uso wangu umejaa aibu tele,
16
kwa ajili ya dhihaka ya wale wanaonilaumu na kunitukana, kwa sababu ya adui, ambaye anatamani kulipiza kisasi.
Settings

Reading Style

Typeface

Font Size 19px

Options