Skip to content
Zaburi 44:1-8

Zaburi 44:1-8

1
Kwa mwimbishaji. Utenzi wa wana wa Kora. Ee Mungu, tumesikia kwa masikio yetu, baba zetu wametueleza yale uliyotenda katika siku zao, siku za kale.
2
Kwa mkono wako uliwafukuza mataifa na ukawapanda baba zetu, uliangamiza mataifa na kuwastawisha baba zetu.
3
Sio kwa upanga wao waliipata nchi, wala si mkono wao uliwapatia ushindi; ilikuwa ni kitanga cha mkono wako wa kuume, na nuru ya uso wako, kwa kuwa uliwapenda.
4
Wewe ni mfalme wangu na Mungu wangu, unayeamuru ushindi kwa Yakobo.
5
Kwa uwezo wako tunawasukuma nyuma watesi wetu; kwa jina lako tunawakanyaga adui zetu.
6
Siutumaini upinde wangu, upanga wangu hauniletei ushindi;
7
bali wewe unatupa ushindi juu ya adui zetu, unawaaibisha watesi wetu.
8
Katika Mungu wetu tunajivuna mchana kutwa, nasi tutalisifu jina lako milele.
Settings

Reading Style

Typeface

Font Size 19px

Options