Rukia maudhui
Zaburi 119:145-152

KOFU: Maombi ya Haraka na Tafakari ya Asubuhi na Mapema

Zaburi 119:145-152
145
Ee Bwana, ninakuita kwa moyo wangu wote, nami nitayatii maagizo yako.
146
Ninakuita; niokoe nami nitazishika sheria zako.
147
Ninaamka asubuhi na mapema na kukuomba msaada; nimeweka tumaini langu katika neno lako.
148
Sikufumba macho yangu usiku kucha, ili niweze kutafakari juu ya ahadi zako.
149
Usikie sauti yangu sawasawa na upendo wako, Ee Bwana, uyahifadhi maisha yangu, sawasawa na sheria zako.
150
Wale wanaopanga mipango miovu wako karibu nami, lakini wako mbali na sheria yako.
151
Ee Bwana, hata hivyo wewe u karibu, na amri zako zote ni za kweli.
152
Tangu zamani nimejifunza kutoka shuhuda zako kwamba umezithibitisha ili zidumu milele.
Settings

Reading Style

Typeface

Font Size 19px

Reading Width 45 chars

Options