Skip to content
Zaburi 119:137-144

Zaburi 119:137-144

137
Ee Bwana, wewe ni mwenye haki, sheria zako ni sahihi.
138
Sheria ulizoziweka ni za haki, ni za kuaminika kikamilifu.
139
Jitihada yangu imenidhoofisha, kwa kuwa adui zangu wanayapuuza maneno yako.
140
Ahadi zako zimejaribiwa kikamilifu, mtumishi wako anazipenda.
141
Ingawa ni mdogo na ninadharauliwa, sisahau mausia yako.
142
Haki yako ni ya milele, na sheria yako ni kweli.
143
Shida na dhiki zimenipata, lakini amri zako ni furaha yangu.
144
Sheria zako ni sahihi milele, hunipa ufahamu ili nipate kuishi.
Settings

Reading Style

Typeface

Font Size 19px

Options