Skip to content
Zaburi 119:129-136

Zaburi 119:129-136

129
Sheria zako ni za ajabu, hivyo ninazitii.
130
Kuingia kwa maneno yako kunaleta nuru, kunampa mjinga ufahamu.
131
Nimefungua kinywa changu na kuhema, nikitamani amri zako.
132
Nigeukie na unihurumie, kama uwafanyiavyo siku zote wale wanaolipenda jina lako.
133
Ongoza hatua zangu kulingana na neno lako, usiache dhambi yoyote initawale.
134
Niokoe na uonevu wa wanadamu, ili niweze kutii mausia yako.
135
Mwangazie mtumishi wako uso wako na unifundishe amri zako.
136
Chemchemi za machozi zinatiririka kutoka machoni yangu, kwa kuwa sheria yako haifuatwi.
Settings

Reading Style

Typeface

Font Size 19px

Options