Zaburi 119:121-128
121
Nimetenda yaliyo haki na sawa, usiniache mikononi mwa watesi wangu.
122
Mhakikishie mtumishi wako usalama, usiache wenye kiburi wanionee.
123
Macho yangu yamefifia, yakitazamia wokovu wako, na kuitazamia ahadi yako ya kweli.
124
Mfanyie mtumishi wako kulingana na upendo wako na unifundishe maagizo yako.
125
Mimi ni mtumishi wako; nipe ufahamu ili niweze kuelewa sheria zako.
126
Ee Bwana, wakati wako wa kutenda umewadia, kwa kuwa sheria yako inavunjwa.
127
Kwa sababu nazipenda amri zako zaidi ya dhahabu, naam, zaidi ya dhahabu safi,
128
na kwa sababu naona maagizo yako yote ni adili, nachukia kila njia potovu.
Settings