Rukia maudhui
Mathayo 26:6-13

Kutiwa Mafuta kwa Yesu huko Bethania

Mathayo 26:6-13
6
Yesu alikuwa Bethania nyumbani mwa Simoni aliyekuwa na ukoma,
7
naye mwanamke mmoja akamjia akiwa na chupa ya marhamu yenye manukato ya thamani kubwa; akayamimina kichwani mwa Yesu alipokuwa ameketi mezani kula chakula.
8
Lakini wanafunzi wake walipoona hayo wakakasirika, wakasema, “Upotevu huu wote ni wa nini?
9
Manukato haya yangeuzwa kwa bei kubwa, na fedha hizo wakapewa maskini.”
10
Yesu, akijua jambo hili, akawaambia, “Mbona mnamsumbua huyu mwanamke? Yeye amenitendea jambo zuri sana.
11
Maskini mtakuwa nao siku zote, lakini mimi hamtakuwa nami siku zote.
12
Alipomiminia haya manukato kwenye mwili wangu, amefanya hivyo ili kuniandaa kwa ajili ya maziko yangu.
13
Amin, nawaambia, mahali popote ulimwenguni ambapo hii Injili itahubiriwa, jambo hili alilolitenda huyu mwanamke litatajwa pia kwa ukumbusho wake.”
Settings

Reading Style

Typeface

Font Size 19px

Reading Width 45 chars

Options