Rukia maudhui
Ayubu 10:8-12

Kitendawili cha kuumbwa na kuangamizwa

Ayubu 10:8-12
8
“Mikono yako ndiyo iliyoniumba na kunifanya. Je, sasa utageuka na kuniangamiza?
9
Kumbuka kuwa ulinifinyanga kama udongo wa mfinyanzi. Je, sasa utanifanya kuwa mavumbi tena?
10
Je, wewe hukunimimina mimi kama maziwa, na kunigandisha kama jibini,
11
ukanivika ngozi na nyama, na kuniunga pamoja kwa mifupa na mishipa?
12
Umenipa uhai na kunitendea wema, katika uangalizi wako umeilinda roho yangu.
Settings

Reading Style

Typeface

Font Size 19px

Reading Width 45 chars

Options