Rukia maudhui
Mwanzo 8:1-5

Mungu ayapunguza maji

Mwanzo 8:1-5
1
Mungu akamkumbuka Noa na wanyama wote wa porini na wa kufugwa waliokuwa naye ndani ya safina, akatuma upepo ukavuma katika dunia, nayo maji yakaondoka.
2
Zile chemchemi zilizo chini sana ya ardhi pamoja na malango ya mafuriko ya mbinguni yakawa yamefungwa nayo mvua ikawa imekoma kunyesha kutoka angani.
3
Maji yakaendelea kupungua taratibu katika nchi. Kunako mwisho wa siku ya 150, maji yalikuwa yamepungua,
4
katika siku ya kumi na saba ya mwezi wa saba, safina ikatua katika milima ya Ararati.
5
Maji yakaendelea kupungua hadi mwezi wa kumi, na siku ya kwanza ya mwezi wa kumi, vilele vya milima vikaonekana.
Settings

Reading Style

Typeface

Font Size 19px

Reading Width 45 chars

Options