Rukia maudhui
Mwanzo 42:1-5

Yakobo Awatuma Wanawe Misri

Mwanzo 42:1-5
1
Wakati Yakobo alipofahamu kuwa kuna nafaka huko Misri, akawaambia wanawe, “Mbona mnakaa tu hapa mnatazamana?”
2
Akaendelea kuwaambia, “Nimesikia kuwa huko Misri kuna nafaka. Telemkeni huko mkanunue chakula kwa ajili yetu, ili tuweze kuishi wala tusife.”
3
Ndipo wale ndugu kumi wa Yosefu, wakateremka huko Misri kununua nafaka.
4
Lakini Yakobo hakumtuma Benyamini, ndugu yake Yosefu, pamoja na wengine, kwa sababu aliogopa asije akapatwa na madhara.
5
Hivyo wana wa Israeli walikuwa miongoni mwa wale waliokwenda Misri kununua nafaka, kwani njaa ilikuwa katika nchi ya Kanaani pia.
Settings

Reading Style

Typeface

Font Size 19px

Reading Width 45 chars

Options