Skip to content
Kutoka 12:43-51

Kutoka 12:43-51

43
Bwana akamwambia Mose na Aroni, “Haya ndiyo masharti kwa ajili ya Pasaka: “Mgeni hataruhusiwa kula Pasaka.
44
Mtumwa yeyote ambaye mmemnunua aweza kuila kama mmemtahiri,
45
lakini kibarua yeyote au msafiri haruhusiwi kula.
46
“Sharti iliwe ndani ya nyumba; msichukue nyama yoyote nje ya nyumba hiyo. Msiuvunje mfupa wowote.
47
Jumuiya yote ya Israeli ni lazima waiadhimishe Pasaka hiyo.
48
“Mgeni aishiye miongoni mwenu ambaye anataka kuadhimisha Pasaka ya Bwana ni lazima wanaume wote waliomo nyumbani mwake wawe wametahiriwa, ndipo aweze kushiriki kama mzawa. Mwanaume yeyote asiyetahiriwa haruhusiwi kuila.
49
Sheria iyo hiyo itamuhusu mzawa na mgeni anayeishi miongoni mwenu.”
50
Waisraeli wote walifanya kama vile Bwana alivyomwagiza Mose na Aroni.
51
Siku ile ile Bwana akawatoa Waisraeli katika nchi ya Misri kwa vikosi vyao.
Settings

Reading Style

Typeface

Font Size 19px

Options