Rukia maudhui

Mithali2

Wito wa Kutafuta Hekima kwa Bidii

1
Mwanangu, kama utayakubali maneno yangu na kuyaweka akiba maagizo yangu ndani mwako,
2
kutega sikio lako kwenye hekima na kuweka moyo wako katika ufahamu,
3
na kama ukiita busara na kuita kwa sauti ufahamu,
4
na kama utaitafuta kama fedha na kuitafuta sana kama hazina iliyofichwa,

Chanzo na Thawabu ya Hekima

5
ndipo utakapoelewa kumcha Bwana na kupata maarifa ya Mungu.
6
Kwa maana Bwana hutoa hekima, na kinywani mwake hutoka maarifa na ufahamu.
7
Anahifadhi ushindi kwa ajili ya mwadilifu, yeye ni ngao kwa wale wasio na lawama,
8
kwa kuwa hulinda mwenendo wa mwenye haki na kuhifadhi njia ya waaminifu wake.
9
Ndipo utafahamu lipi lililo kweli na haki na sawa: yaani kila njia nzuri.
10
Kwa maana hekima itaingia moyoni mwako, nayo maarifa yataifurahisha nafsi yako.
11
Busara itakuhifadhi na ufahamu utakulinda.

Hekima Huwalinda na Watu Waovu

12
Hekima itakuokoa kutoka njia za waovu, kutoka kwa watu ambao maneno yao yamepotoka,
13
wale waachao mapito yaliyonyooka wakatembea katika njia za giza,
14
wale wapendao kutenda mabaya na kufurahia upotovu wa ubaya,
15
ambao mapito yao yamepotoka na ambao ni wapotovu katika njia zao.

Hekima Huwalinda na Mwanamke Mzinzi

16
Itakuokoa pia kutokana na mwanamke kahaba, kutokana na mke aliyepotoka mwenye maneno ya kushawishi kutenda ubaya,
17
aliyemwacha mwenzi wa ujana wake na kupuuza agano alilofanya mbele ya Mungu.
18
Kwa maana nyumba yake huelekea kwenye kifo na mapito yake kwenye roho za waliokufa.
19
Hakuna yeyote aendaye kwake akarudi, au kufikia mapito ya uzima.

Hatima ya Njia Mbili

20
Hivyo utatembea katika njia za watu wema na kushikamana na mapito ya wenye haki.
21
Kwa maana wanyofu wataishi katika nchi, nao wasio na lawama watabakia ndani yake.
22
Bali waovu watakatiliwa mbali kutoka nchi, nao wasio waaminifu watangʼolewa kutoka humo.
Use arrow keys to navigate
Settings

Reading Style

Typeface

Font Size 19px

Reading Width 45 chars

Options