Rukia maudhui

Mistari ya Biblia kuhusu Tribe Of Benjamin

107 mistari · 35 vipengele

Mistari muhimu ya Biblia

Chuja kwa kitabu
  1. Hawa ndio watu waliomjia Daudi huko Siklagi, wakati alikuwa amefukuzwa mbele ya Sauli mwana wa Kishi (walikuwa miongoni mwa mashujaa waliomsaidia Daudi vitani,

  2. walikuwa na pinde na walikuwa na uwezo wa kupiga mishale au kutupa mawe kwa kombeo wakitumia mkono wa kushoto au wa kulia; hawa walikuwa ndugu zake Sauli kutoka kabila la Benyamini):

  3. Mkuu wao alikuwa Ahiezeri, na wa pili Yoashi, wote wana wa Shemaa Mgibeathi; pia Yezieli na Peleti wana wa Azmawethi; Beraka, Yehu Mwanathothi,

  4. na Ishmaya Mgibeoni, shujaa miongoni mwa wale Thelathini, ambaye alikuwa kiongozi wa wale Thelathini; Yeremia, Yahazieli, Yohanani, Yozabadi, Mgederathi,

  5. Eluzai, Yeremothi, Bealia, Shemaria, Shefatia, Mharufi;

  6. Elikana, Ishia, Azareli, Yoezeri na Yashobeamu, wana wa Kora;

  7. Yoela na Zebadia, wana wa Yerohamu, kutoka Gedori.