Skip to content

Mistari ya Biblia kuhusu The High Priest: Interceding

6 mistari · 65 vipengele

Mistari kuhusu Interceding

  1. Ndipo Mose na Aroni wakaenda mbele ya Hema la Kukutania,

  2. naye Bwana akamwambia Mose,

  3. “Jitenge mbali na kusanyiko hili ili niweze kuwaangamiza mara moja.” Wakaanguka chini kifudifudi.

  4. Kisha Mose akamwambia Aroni, “Chukua chetezo chako na uweke uvumba ndani yake, pamoja na moto kutoka madhabahuni, nawe uende haraka kwenye kusanyiko ili kufanya upatanisho kwa ajili yao. Ghadhabu imekuja kutoka kwa Bwana, na tauni imeanza.”

  5. Hivyo Aroni akafanya kama Mose alivyosema, akakimbilia katikati ya kusanyiko. Tauni ilikuwa tayari imeanza miongoni mwa watu, lakini Aroni akafukiza uvumba na kufanya upatanisho kwa ajili yao.

  6. Aroni akasimama kati ya waliokuwa hai na waliokufa, nayo tauni ikakoma.