Rukia maudhui

Mistari ya Biblia kuhusu Prosperity

31 mistari · 8 vipengele

Mistari muhimu ya Biblia

Chuja kwa kitabu
  1. Wimbo wa kwenda juu. Heri ni wale wote wamchao Bwana, waendao katika njia zake.

  2. Utakula matunda ya kazi yako; baraka na mafanikio vitakuwa vyako.

  3. Nyakati zikiwa nzuri, ufurahi, lakini nyakati zikiwa mbaya, tafakari: Mungu amefanya hiyo moja, naam, sanjari na hiyo nyingine. Kwa hiyo, mwanadamu hawezi kugundua kitu chochote kuhusu maisha yake ya baadaye.

  4. “Kwa nini niwasamehe? Watoto wenu wameniacha na kuapa kwa miungu ambayo si miungu. Niliwapatia mahitaji yao yote, lakini bado wamefanya uzinzi na kusongana katika nyumba za makahaba.

  5. Kadiri makuhani walivyoongezeka, ndivyo walivyozidi kutenda dhambi dhidi yangu, walibadilisha utukufu wao kwa kitu cha aibu.

  6. Nilipowalisha, walishiba, waliposhiba, wakajivuna, kisha wakanisahau mimi.