Rukia maudhui

Mistari ya Biblia kuhusu Nation: Peace given by God

7 mistari · 11 vipengele

Mistari kuhusu Peace given by God

  1. Bwana akawapa pumziko kila upande, kama vile alivyokuwa amewaapia baba zao, hakuna hata mmoja wa adui zao aliyeweza kusimama mbele yao, Bwana akawatia adui zao wote mikononi mwao.

  2. Akawaambia, “Je, Bwana Mungu wenu si yuko pamoja na ninyi? Pia si amewapa raha pande zote? Kwa maana amewatia wenyeji wa nchi mkononi mwangu, nayo nchi iko chini ya Bwana na watu wake.

  3. Kwa maana Daudi alikuwa amesema, “Kwa vile Bwana, Mungu wa Israeli amewapa watu wake raha na amekuja kuishi Yerusalemu milele,

  4. kwa maana huimarisha makomeo ya malango yako na huwabariki watu wako walio ndani yako.

  5. Huwapa amani mipakani mwenu na kukushibisha kwa ngano safi kabisa.

  6. wakati wa kupenda na wakati wa kuchukia, wakati wa vita na wakati wa amani.

  7. Mimi ninaumba nuru na kuhuluku giza, ninaleta mafanikio na kusababisha maafa. Mimi, Bwana, huyatenda haya yote.