Rukia maudhui

Mistari ya Biblia kuhusu Commerce: Carried on by means of ships

10 mistari · 64 vipengele

Mistari kuhusu Carried on by means of ships

  1. Naye Hiramu akawatuma watu wake; mabaharia walioijua bahari, kuhudumu katika hizo meli pamoja na watu wa Solomoni.

  2. Wakasafiri kwa bahari mpaka Ofiri na kurudi na talanta 420 za dhahabu, ambazo walimkabidhi Mfalme Solomoni.

  3. Wengine walisafiri baharini kwa meli, walikuwa wafanyabiashara kwenye maji makuu.

  4. Waliziona kazi za Bwana, matendo yake ya ajabu kilindini.

  5. Kwa maana alisema na kuamsha tufani iliyoinua mawimbi juu.

  6. Yakainuka juu mbinguni, yakashuka chini hadi vilindini, katika hatari hii ujasiri wao uliyeyuka.

  7. Walipepesuka na kuyumbayumba kama walevi, ujanja wao ukafikia ukomo.

  8. Ndipo walipomlilia Bwana katika shida yao, naye akawatoa kwenye taabu yao.

  9. Akatuliza dhoruba kwa mnongʼono, mawimbi ya bahari yakatulia.

  10. Walifurahi ilipokuwa shwari, naye akawaongoza hadi bandari waliyoitamani.