Skip to content

Bozrah

7 verses

30.7300, 35.6000 Tazama kwenye Ramani za Google

Mistari inayomtaja Bozrah

  1. Bela alipofariki, Yobabu mwana wa Zera kutoka Bosra akawa mfalme baada yake.

  2. Bela alipofariki, Yobabu mwana wa Zera kutoka Bosra akawa mfalme baada yake.

  3. Upanga wa Bwana umeoga katika damu, umefunikwa na mafuta ya nyama: damu ya kondoo na mbuzi, mafuta kutoka figo za kondoo dume. Kwa maana Bwana ana dhabihu huko Bosra, na machinjo makuu huko Edomu.

  4. Ni nani huyu anayekuja kutoka Edomu, kutoka Bosra, mwenye mavazi yaliyotiwa madoa mekundu? Ni nani huyu, aliyevikwa joho la kifahari, anayetembea kwa ukuu wa nguvu zake? “Mimi ndimi, nisemaye katika haki, mwenye nguvu wa kuokoa.”

  5. Ninaapa kwa nafsi yangu,” asema Bwana, “kwamba Bosra utakuwa magofu na kitu cha kutisha, cha aibu na cha kulaania; miji yake yote itakuwa magofu milele.”

  6. Tazama! Tai atapaa juu angani na kuruka chini kwa ghafula, akitandaza mabawa yake juu ya Bosra. Katika siku hiyo, mioyo ya mashujaa wa Edomu itakuwa kama moyo wa mwanamke katika utungu wa kuzaa.

  7. Nitatuma moto juu ya Temani ambao utateketeza ngome za Bosra.”