Rukia maudhui
Zaburi 65:1-4

Sifa, Upatanisho na Kumkaribia Mungu

Zaburi 65:1-4
1
Kwa mwimbishaji. Zaburi ya Daudi. Wimbo. Ee Mungu, sifa zakungojea katika Sayuni; kwako wewe nadhiri zetu zitatimizwa.
2
Ewe usikiaye maombi, kwako wewe watu wote watakuja.
3
Tulipokuwa tumefunikwa kabisa na dhambi, wewe ulisamehe makosa yetu.
4
Heri wale uliowachagua na kuwaleta karibu ili waishi katika nyua zako! Tunashibishwa kwa mema ya nyumba yako, mema ya Hekalu lako takatifu.
Settings

Reading Style

Typeface

Font Size 19px

Reading Width 45 chars

Options