Skip to content
Zaburi 44:17-26

Zaburi 44:17-26

17
Hayo yote yametutokea, ingawa tulikuwa hatujakusahau wala hatujaenda kinyume na agano lako.
18
Mioyo yetu ilikuwa haijarudi nyuma; nyayo zetu zilikuwa hazijaiacha njia yako.
19
Lakini ulituponda na kutufanya makao ya mbweha, na ukatufunika kwa giza nene.
20
Kama tungalikuwa tumelisahau jina la Mungu wetu au kunyooshea mikono yetu kwa mungu mgeni,
21
je, Mungu hangaligundua hili, kwa kuwa anazijua siri za moyo?
22
Hata hivyo kwa ajili yako tunauawa mchana kutwa; tumehesabiwa kama kondoo wa kuchinjwa.
23
Amka, Ee Bwana! Kwa nini unalala? Zinduka! Usitukatae milele.
24
Kwa nini unauficha uso wako na kusahau taabu na mateso yetu?
25
Tumeshushwa hadi mavumbini, miili yetu imegandamana na ardhi.
26
Inuka na utusaidie, utukomboe kwa sababu ya upendo wako usio na mwisho.
Settings

Reading Style

Typeface

Font Size 19px

Options