23
Amka, Ee Bwana! Kwa nini unalala? Zinduka! Usitukatae milele.
24
Kwa nini unauficha uso wako na kusahau taabu na mateso yetu?
25
Tumeshushwa hadi mavumbini, miili yetu imegandamana na ardhi.
26
Inuka na utusaidie, utukomboe kwa sababu ya upendo wako usio na mwisho.