Skip to content
Zaburi 45:1

Zaburi 45:1

Inaonyesha mstari 1 pamoja na muktadha unaouzunguka.
1
Kwa mwimbishaji. Mtindo wa utenzi wa “Yungiyungi.” Utenzi wa wana wa Kora. Wimbo wa arusi. Moyo wangu umesisimuliwa na jambo jema ninapomsimulia mfalme mabeti yangu; ulimi wangu ni kalamu ya mwandishi stadi.
2
Wewe ni bora kuliko watu wengine wote na midomo yako imepakwa neema, kwa kuwa Mungu amekubariki milele.
3
Jifunge upanga wako pajani mwako, ee mwenye nguvu, jivike fahari na utukufu.
4
Katika fahari yako, songa mbele kwa ushindi, kwa ajili ya kweli, unyenyekevu na haki, mkono wako wa kuume na uonyeshe matendo ya kutisha.
Settings

Reading Style

Typeface

Font Size 19px

Options