Skip to content
Zaburi 17:1-5

Ombi la Kusikilizwa kwa Haki

Zaburi 17:1-5
1
Sala ya Daudi. Sikia, Ee Bwana, kusihi kwangu kwa haki, sikiliza kilio changu. Tega sikio kwa ombi langu, halitoki kwenye midomo ya udanganyifu.
2
Hukumu yangu na itoke kwako, macho yako na yaone yale yaliyo haki.
3
Ingawa unauchunguza moyo wangu na kunikagua usiku, ingawa umenijaribu, hutaona chochote. Nimeamua kwamba kinywa changu hakitatenda dhambi.
4
Kuhusu matendo ya wanadamu: kwa neno la midomo yako, nimejiepusha na njia za wenye jeuri.
5
Hatua zangu zimeshikamana na njia zako; nyayo zangu hazikuteleza.
Settings

Reading Style

Typeface

Font Size 19px

Options