Skip to content
Mithali 26:17-22

Mithali 26:17-22

17
Kama yeye amkamataye mbwa kwa masikio, ndivyo alivyo mtu apitaye njiani na kujiingiza kwenye ugomvi usiomhusu.
18
Kama mtu mwendawazimu atupaye vijinga vya moto au mishale ya kufisha,
19
ndivyo alivyo mtu amdanganyaye jirani yake na kusema, “Nilikuwa nikifanya mzaha tu!”
20
Bila kuni moto huzimika; pasipo uchongezi ugomvi humalizika.
21
Kama makaa juu ya makaa yanayowaka, na kama kuni kwenye moto, ndivyo alivyo mtu mgomvi kwa kuchochea ugomvi.
22
Maneno ya mchongezi ni kama chakula kitamu; huingia sehemu za ndani sana za mtu.
Settings

Reading Style

Typeface

Font Size 19px

Options