Rukia maudhui
Mithali 15:25-29

Hukumu na Ulinzi wa Mungu

Mithali 15:25-29
25
Bwana hubomoa nyumba ya mtu mwenye kiburi, bali huilinda mipaka ya mjane isiguswe.
26
Bwana huchukia sana mawazo ya mwovu, bali mawazo ya wale walio safi humfurahisha yeye.
27
Mtu mwenye tamaa huletea jamaa yake taabu, bali yeye achukiaye rushwa ataishi.
28
Moyo wa mwenye haki hupima majibu yake, bali kinywa cha mwovu hufoka ubaya.
29
Bwana yuko mbali na waovu, bali husikia maombi ya wenye haki.
Settings

Reading Style

Typeface

Font Size 19px

Reading Width 45 chars

Options