Mithali 15:30-33
30
Mtazamo wa tabasamu huleta furaha moyoni, nazo habari njema huipa mifupa afya.
31
Yeye asikilizaye maonyo yatoayo uzima atakuwa miongoni mwa wenye hekima.
32
Yeye anayedharau maonyo hujidharau mwenyewe, bali yeyote anayekubali maonyo hupata ufahamu.
33
Kumcha Bwana humfundisha mtu hekima, nao unyenyekevu huja kabla ya heshima.
Settings