Skip to content
Hesabu 32:33-38

Hesabu 32:33-38

33
Kisha Mose akawapa Wagadi, Wareubeni, na nusu ya kabila la Manase mwana wa Yosefu ufalme wa Sihoni mfalme wa Waamori, na ufalme wa Ogu mfalme wa Bashani, nchi yote pamoja na miji yake, na nchi inayowazunguka.
34
Wagadi wakajenga Diboni, Atarothi, Aroeri,
35
Atroth-Shofani, Yazeri, Yogbeha,
36
Beth-Nimra na Beth-Harani kama miji iliyozungushiwa ngome, tena wakajenga mazizi kwa ajili ya makundi yao ya mbuzi na kondoo.
37
Nao Wareubeni wakajenga upya miji ya Heshboni, Eleale na Kiriathaimu,
38
pia Nebo na Baal-Meoni (majina ya hiyo miji yalibadilishwa) na Sibma. Miji waliyoijenga upya waliipa majina.
Settings

Reading Style

Typeface

Font Size 19px

Options