Rukia maudhui
Marko 14:17-21

Yesu Atabiri Kusalitiwa Kwake

Marko 14:17-21
17
Ilipofika jioni, Yesu akaja pamoja na wale wanafunzi wake kumi na wawili.
18
Walipoketi mezani wakila, Yesu akawaambia, “Amin, nawaambia, mmoja wenu atanisaliti, mmoja anayekula pamoja nami.”
19
Wakaanza kuhuzunika na kumuuliza mmoja baada ya mwingine, “Je, ni mimi Bwana?”
20
Akawajibu, “Ni mmoja miongoni mwenu ninyi kumi na wawili, yule anayechovya mkate kwenye bakuli pamoja nami.
21
Mwana wa Adamu anaenda zake kama vile alivyoandikiwa. Lakini ole wake mtu yule amsalitiye Mwana wa Adamu! Ingekuwa heri kwake mtu huyo kama hangezaliwa.”
Settings

Reading Style

Typeface

Font Size 19px

Reading Width 45 chars

Options