Skip to content
Waamuzi 9:1

Waamuzi 9:1

Inaonyesha mstari 1 pamoja na muktadha unaouzunguka.

Abimeleki Atafuta Ufalme huko Shekemu

1
Siku moja Abimeleki mwana wa Yerub-Baali akaenda kwa ndugu ya mama yake huko Shekemu na kuwaambia yeye na ukoo wote wa mama yake,
2
“Waulizeni watu wote wa Shekemu, ‘Lipi lililo bora kwenu: Kutawaliwa na wana wote sabini wa Yerub-Baali, au mtu mmoja peke yake?’ Kumbukeni kwamba, mimi ni mfupa wenu nyama yenu hasa.”
3
Ndugu za mama yake walipowaeleza watu wote wa Shekemu, wakaelekea kumkubali Abimeleki, kwa kuwa walisema, “Yeye ni ndugu yetu.”
4
Wakampa shekeli sabini za fedha kutoka hekalu la Baal-Berithi, naye Abimeleki akaitumia kuajiri watu ovyo wasiojali, wakawa ndio wafuasi wake.

Jifunze kifungu hiki

Ufafanuzi wa kifungu hiki, si mstari mmoja.

Maandiko mengine yanaposema hivi.

  • Waamuzi 8:31

    Suria wake, aliyekuwa anaishi huko Shekemu, pia alimzalia mwana, ambaye alimwita Abimeleki.
    kutoka mstari wa 1
  • Zaburi 83:2

    Tazama watesi wako wanafanya fujo, jinsi adui zako wanavyoinua vichwa vyao.
    kutoka mstari wa 1
  • Zaburi 83:4

    Wanasema, “Njooni, tuwaangamize kama taifa, ili jina la Israeli lisikumbukwe tena.”
    kutoka mstari wa 1
  • 1 Wafalme 12:1

    Rehoboamu akaenda Shekemu, kwa kuwa Waisraeli wote walikuwa wamekwenda huko kumfanya yeye kuwa mfalme.
    kutoka mstari wa 1
  • 1 Wafalme 12:3

    Kwa hiyo wakatuma watu kumwita Yeroboamu, yeye na kusanyiko lote la Israeli wakamwendea Rehoboamu na kumwambia,
    kutoka mstari wa 1
  • 1 Wafalme 12:20

    Waisraeli wote waliposikia kwamba Yeroboamu amerudi, wakatuma watu na kumwita kwenye kusanyiko na kumfanya mfalme juu ya Israeli yote. Ni kabila la Yuda peke yake lililobaki kuwa tiifu kwa nyumba ya Daudi.
    kutoka mstari wa 1
  • 2 Samweli 15:6

    Absalomu akaendelea na tabia hii mbele ya Waisraeli wote waliomjia mfalme kumwomba awape haki; kwa hiyo Absalomu akaiba mioyo ya watu wa Israeli.
    kutoka mstari wa 1
  • Mwanzo 33:18

    Baada ya Yakobo kutoka Padan-Aramu, alifika salama katika mji wa Shekemu huko Kanaani na kuweka kambi yake karibu na mji.
    kutoka mstari wa 1
  • Mwanzo 34:2

    Ikawa Shekemu mwana wa Hamori Mhivi, mtawala wa eneo lile alipomwona, akamchukua na kumnajisi.
    kutoka mstari wa 1
  • Yeremia 18:18

    Wakasema, “Njooni, tutunge hila dhidi ya Yeremia; kwa kuwa kufundisha sheria kwa kuhani hakutapotea, wala shauri litokalo kwa mwenye hekima, wala neno la manabii. Hivyo njooni, tumshambulie kwa ndimi zetu na tusijali chochote asemacho.”
    kutoka mstari wa 1
Settings

Reading Style

Typeface

Font Size 19px

Options