Rukia maudhui
Ayubu 27:5-12

Kiapo cha uadilifu

Ayubu 27:5-12
5
Sitakubaliana nanyi kabisa kuwa mko sahihi; hadi nife, sitakana uadilifu wangu.
6
Nitadumisha haki yangu wala sitaiacha; dhamiri yangu haitanisuta muda wote ninaoishi.
7
“Watesi wangu wawe kama waovu, nao adui zangu wawe kama wasio haki!
8
Kwa maana mtu asiyemcha Mungu analo tegemeo gani anapokatiliwa mbali, Mungu anapouondoa uhai wake?
9
Je, Mungu husikiliza kilio chake, shida zimjiapo?
10
Je, anaweza kumfurahia Mwenyezi? Je, atamwita Mungu nyakati zote?
11
“Nitawafundisha juu ya uweza wa Mungu; njia za Mwenyezi sitazificha.
12
Ninyi nyote mmeona hili wenyewe. Ni ya nini basi mazungumzo haya yasiyo na maana?
Settings

Reading Style

Typeface

Font Size 19px

Reading Width 45 chars

Options