Skip to content
Ayubu 13:1-12

Ayubu 13:1-12

1
“Macho yangu yameona hili lote, masikio yangu yamesikia na kulielewa.
2
Hayo mnayoyajua mimi pia ninayajua; mimi si mtu duni kuliko ninyi.
3
Lakini ninayo shauku ya kuzungumza na Mwenyezi na kuhojiana shauri langu na Mungu.
4
Ninyi, hata hivyo, hunipakaza uongo; ninyi ni matabibu wasiofaa kitu, ninyi nyote!
5
Laiti wote mngenyamaza kimya! Kwa kuwa kwenu hilo lingekuwa hekima.
6
Sikieni sasa hoja yangu; sikilizeni kusihi kwangu.
7
Je, mtazungumza kwa uovu kwa niaba ya Mungu? Je, mtazungumza kwa udanganyifu kwa niaba yake?
8
Mtamwonyesha upendeleo? Mtamtetea Mungu kwenye mashtaka yake?
9
Je, ingekuwa vyema Mungu akiwahoji ninyi? Je, mngeweza kumdanganya kama ambavyo mngeweza kuwadanganya wanadamu?
10
Hakika angewakemea kama mkiwapendelea watu kwa siri.
11
Je, huo ukuu wake haungewatisha ninyi? Je, hofu yake isingewaangukia ninyi?
12
Maneno yenu ni mithali za majivu; utetezi wenu ni ngome za udongo wa mfinyanzi.
Settings

Reading Style

Typeface

Font Size 19px

Options