Skip to content
Ayubu 12:13-25

Ayubu 12:13-25

13
“Hekima na nguvu ni vya Mungu; shauri na ufahamu ni vyake yeye.
14
Kile anachokibomoa hakiwezi kujengeka tena; mtu aliyefungiwa naye hawezi kufunguliwa.
15
Akizuia maji, huwa pana ukame; akiyaachia maji, huharibu nchi.
16
Kwake kuna nguvu na ushindi; adanganywaye na adanganyaye, wote wawili ni wake.
17
Yeye huwaondoa washauri wakiwa wametekwa nyara, naye huwapumbaza wanaotoa maamuzi.
18
Huondoa pingu zilizofungwa na wafalme, na kuwafunga mishipi ya kiunoni.
19
Huwaondoa makuhani wakiwa wametekwa nyara, na kuwaangusha waliojiimarisha muda mrefu.
20
Hunyamazisha midomo ya washauri wanaoaminika, na kuondoa busara ya wazee.
21
Huwamwagia dharau wanaoheshimika, na kuwavua silaha wenye nguvu.
22
Hufunua mambo ya ndani ya gizani, na kuyaleta nuruni yale yaliyositirika sana.
23
Huyafanya mataifa yatukuke na kuyaangamiza; hufanya mataifa kuwa makubwa, naye huyatawanya.
24
Huwaondolea viongozi wa nchi akili zao; huwapeleka watangetange nyikani pasipo na njia.
25
Hupapasa gizani pasipokuwa na mwanga; huwafanya wapepesuke kama walevi.
Settings

Reading Style

Typeface

Font Size 19px

Options