Ayubu 12:7-12
7
“Lakini ulizeni wanyama, nao watawafundisha, au ndege wa angani, nao watawaambia;
8
au zungumzeni na dunia, nayo itawafundisha, au acheni samaki wa baharini wawape taarifa.
9
Ni nani miongoni mwa hawa wote asiyejua kwamba mkono wa Bwana ndio uliofanya hili?
10
Mkononi mwake kuna uhai wa kila kiumbe, na pumzi ya wanadamu wote.
11
Je, sikio haliyajaribu maneno kama vile ulimi uonjavyo chakula?
12
Je, hekima haipatikani katikati ya wazee? Je, maisha marefu hayaleti ufahamu?
Settings